Makonda ataja majina mapya 65 ya watuhumiwa dawa za kulevya, Mbowe, Gwajima, Iddi Azan, Manji wamo Ndani ya Dishi

 
Makonda katika picha akiwa na waandishi wa habari
 Akiwa katika awamu ya pili ya kupambana na Biashara ya madawa ya kulevya Makonda ameagiza: Wafuatao (Watu 65) wakutane katika kituo cha kati cha Polisi cha Kanda maalumu ya Dar es salaam Siku ya Ijumaa ambapo miongoni mwao ni, Aikaeli Mbowe (Mbunge wa Hai), Mchungaji Gwajima (Kanisa la Ufufuo na Uzima), Yusuph Manji (M/kiti Yanga), Mmiliki wa Slipway ambae analo eneo la kupaki boti, mmliki wa yatchclub, mmiliki wa MMI, Mwinyi Machata, Rose ambae ana mtandao mpana, Kiboko, Mbunge mstaafu Iddi Azan, Hussein Pamba kali.
 
Kuhusu ishu ya Agness Masogange iliyosemwa na Wema Sepetu? Paul Makonda amejibu hivi:

"Mimi nina kifua cha kuhimili mikiki yote, kwa hiyo ni kama ina niongezea nguvu, sasa wewe umekamatwa unashindwaje kumtaja muhusika akakamatwa na uko sehemu husika? Hata hivyo mtu ukiwa mahabusu unawezaje kutumia simu? Hilo ni kosa na sasa vyombo vya usalama vina lishughulikia hilo"
‘Haya mengine yanaoendelea kama mtu ana ushahidi anatupa taarifa tumekamata  watu zaidi 120 kupitia taarifa tulizozipata sasa wewe umeshindwaje kumtaja naye akafuatwa’

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »