|  | 
| Kikosi cha Yanga kilicho ivuruga Ngaya Leo | 
YANGA SC wameanza vizuri mawindo yao ya ubingwa wa Afrika, baada ya 
kwachapa wenyeji Ngaya Club de Mde mabao 5-1 jioni ya leo mjini Moroni, 
Comoro.
Ushindi huo unamaanisha Yanga watakuwa na shughuli nyepesi tu katika 
mchezo wa marudiano wiki ijayo mjini Dar es Salaam, kwani hata 
wakifungwa 3-0 watasonga mbele.
Kiungo Mzambia, Justin Zulu alifungua akaunti yake ya mabao Jangwani 
baada ya kusajiliwa msimu huu kwa kuifungia Yanga bao la kwanza dakika 
ya 43.
Winga machachari, Simon Msuva akaifungia Yanga bao la pili 
dakika ya 45 na Yanga ikaenda kupumzika inaongoza kwa mabao 2-0.
Mzambia mwingine, Obrey Chirwa akaifungia Yanga bao la tatu dakika ya 
59, kabla ya Mrundi, Amissi Tambwe kufunga la nne dakika ya 65 
na Mzimbabwe Thabani Kamusoko kufunga la tano dakika ya 73.
Ngaya walijipatia bao lao la kufutia machozi dakika ya 66 kupitia kwa 
Said Anfane  Mohammed aliyetokea benchi kipindi cha pili.
Kikosi cha Ngaya kilikuwa; Said Mmadi, Said Hachim, Said Tothir, 
Adhepeau Denis Hubert, Ali Ahmada, Youssouf Ibrahim Moidjie, Zamir 
Mohammed, Mounir Moussa, Franck Said Abderemane, Rakoarimanana 
Falinurina na Chadhuili Mradabi.
Yanga SC; Deogratius Munishi ‘Dida’, Juma Abdul, Mwinyi Hajji, Nadir 
Haroub ‘Cannavaro’, Kevin Yondan, Justin Zullu, Simoni Msuva/Emmanuel 
Martin, Thabani Kamusoko, Amissi Tambwe/Juma Mahadhi, Obrey Chirwa na 
Haruna Niyonzima/Said Juma ‘Maka
